٣٩

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
٤٠
Ila waja wako walio safika.
٤١
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
٤٢
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
Notes placeholders