Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
059

Sura Al-Hashr

Aya:

24

Mahali iliteremshwa:

Madina

SURAT AL-H'ASHRI 

(Imeteremka Madina)

 Sura imeanzia kwa kutoa khabari kwamba kila kitu kilioko katika mbingu na ardhi kinamsabihi na kinamtakasa Mwenyezi mungu na kila kitu ambacho si laiki naye. Na kwamba Yeye ni Mtukufu Mwenye nguvu asiye shindika, ni Mwenye hikima katika kuendesha kwake na kupanga kwake Sharia. Na katika matokeo ya nguvu zake na hikima yake ni yale yanayo simuliwa na Sura hii yaliyo wapata Bani Nnadhiiri, nao ni katika Mayahudi wa Madina. Walikuwa hao walisuluhiana na Mtume s.a.w baada.ya kuhamia Madina kwamba wasiwe dhidi yake wala upande wake. Walipo shindwa Waislamu katika vita vya Uhud, walivunja agano lao wakaungana na Maqureshi dhidi ya Mtume s.a.w. Hapo ndipo akenda akawazunguka katika ngome zao ambazo walidhani wenyewe kuwa zitawalinda, na zisiweze kuwalinda. Tena ndio akawafukuza kutoka Madina. 

Kisha Sura inaeleza hukumu ya mali yaliyo patikana kwa maadui bila ya kupigana vita wala kukimbilia kwa farasi na kadhaalika. Ikataja kuwa hayo ni ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na jamaa, na mayatima, na masikini, na wasafiri, na mafakiri katika wakimbizi walio tolewa kwenye nyumba zao na mali yao. Kisha Sura ikasimulia khabari za Ansari, Waislamu wa Madina, na fadhila yao, na jinsi walivyo kuwa wanawafadhilisha Wahajiri, wakimbizi, kuliko nafsi zao, ijapo kuwa wao wenyewe wana haja ya hivyo wanavyo toa. Na Sura inataka macho yaangalie zile ahadi za wanaafiki kwa Bani Nnadhiiri, na kauli yao waliyo sema: Pindi mkitolewa, nasi tutatoka pamoja nanyi! Na mkipigwa vita tutakusaidieni! Basi Sura imeufedhehi uwongo wao huo, udanganyifu wao katika hayo. 

Kisha Sura ikamalizikia kwa kuwakumbusha Waumini kwa yatakikanayo wawe nayo nayo ni kumcha Mwenyezi Mungu, na kujiwekea akiba kwa siku zijazo za karibuni na mbali. Na wala wasiwe kama wale walio mpuuza Mwenyezi Mungu, nay akawasahaulisha nafsi zao. 

Na ikakhitimisha Sura kwa kubainisha hadhi ya Qur'ani na ubora wa taathira yake. Hayo ni hivyo kwa sababu aliye iteremsha ni Yeye Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu isipo kuwa Yeye Mwenye Asmau-l-Husna, Majina Mazuri kabisa.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa