Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
017

Sura Bani Israil

Aya:

111

Mahali iliteremshwa:

Makka

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURA AL ISRAAI (BANI ISRAIL)  

(Imeteremka Makka)

Sura hii tukufu ina Aya 111, nayo ni Sura ya Makka ila Aya hizi: 26, 32, 33, 57 na tangu Aya 73 mpaka Aya 80. Aya zote hizi. nazo ni 12, ni za Madina. Sura hii imeanza kwa kumsabihi, kumtakasa, Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kisha ikaitaja Israi, nayo ni safari ya usiku aliyo chukuliwa Mtume s.a.w. kutoka Makka mpaka Bait Al Muqaddas (Yerusalemu), na baadae akapelekwa mbinguni, na kurejeshwa Makka usiku ule ule.

Baadae Sura inaeleza Ujumbe wa Nabii Musa (AS), na yaliyo kuwa ya Wana wa Israili Kisha ikaashiria cheo cha Qur’ani Tukufu katika uwongofu, na zikatajwa Aya za uumbaji usiku na mchana, na yatakayo watokea watu Siku ya Kiyama katika kulipwa kwa vitendo walivyo vitenda duniani. Na Subhanahu amebainisha sababu ze kuharibika umma, na hali ya watu katika kuhangaika kwao, na matokeo ya vitenda vyao huko Akhera. Tena zikaja Aya za kutukuzwa wazazi, baba na mama, na hali ya watu kukhusu mali zao; na zikaja Amri Kumi za kuunda umma ulio bora. Kisha Subhanahu akauvunja uzushi wa washirikina kukhusu Malaika, kisha akabainisha Qur'ani inavyo eleza hoja zake. 

Kisha Subhanahu akaashiria anavyo stahiki kuhimidiwa, na upinzani wa washirikina, akawapa wasia Waumini. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu akaeleza namna anavyo watendea makafiri duniani na Akhera. Tena akaeleza asili ya uumbaji wa binaadamu na Shetani, na akawatisha washirikina kwa Aya zake. Baada ya hayo, Subhanahu alibainisha utukufu wa binaadamu, na akataja adhabu za Siku ya Kiyama. Akataja vipi washirikina wanavyo jaribu kumzuia Nabi asitimize Wito wake, na vipi Mwenyezi Mungu anavyomtia nguvu. Baada ya hayo Allahu Subhanahu wa Taa'la akamuusia Nabii kwa wasia za uwongofu, na wito mnasaba. Kisha akaashiria cheo cha Qur`ani Tukufu. na akataja khabari za Roho, na akaashiria siri zake. Kisha akataja umuujiza wa Qur'ani, kushindwa majini na watu kuleta mfano wake. Na akabainisha Subhanahu uwezo wake kuleta Ishara nyengine. Tena akataja vipi Qur’ani ilivyo kusanya Haki; na hali za Waumini wema katika Imani zao, na inavyo takikana kuwa daima wawe wanamhimidi Mwenyezi Mungu na wakimtukuza. 

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa