🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
033

Sura Al-Ahzab

Aya:

73

Mahali iliteremshwa:

Madina

SURAT AL-AH'ZAB 

(Imeteremka Madina)

Sura hii imeanza kwa kumtaka Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w. amche Mwenyezi Mungu na amtegemee Yeye. Tena ikaingia kuzungumza juu ya mas-ala ya watoto wa kupanga na ikakataa kuwa hao wana wanao walea kuwa ni watoto wao khasa. Na  ikataja mapenzi na utiifu wa Mwenyezi Mungu alio wajibisha kwa ajili ya Mtume wake, na hishima na kuwatukuza Mamama wa Waumini, yaani wake za Mtume. Na  Sura imeeleza ahadi aliyo ichukua Mwenyezi Mungu kwa Manabii kuwa wafikishe ujumbe; na ikafafanua khabari za Vita vya Ah'zab (Makundi) na khofu na misukosuko iliyo kuwako, na vipi mwishoe Waumini wakashinda na ahadi ya Mwenyezi Mungu ikatimia. 

Na Sura hii ikashughulikia kutaja adabu ambazo zinawapasa wake za Mtume kuzifuata, na wajilazimishe nafsi zao kuzishika. Tena ikaangukia kuzungumza juu ya watoto wa kupanga. Na ikavunja ada ya siku za kijahiliya, za ujinga, ilipo kuwa  kuharimisha mtu kuoana na mwana wa kupanga ambaye kwa hakika ni halali yake. Na Sura ikamsifu Mtume s.a.w. na ikamthibitishia aliyo kuwa anastahiki. Na ikausia kustareheshwa na kumwacha kwa wema mwanamke anaye pewa talaka kabla ya kuingia harusi. Na ikamkhusisha Mtume s.a.w. kuwa imemhalalishia mwanamke aliye jitolea kuolewa naye, na ikasema wazi kuwa si halali kwake kuzidisha kuowa wanawake wengine baada ya hao tisa alio kuwa nao. 

Kisha Sura tukufu ikabainisha yanayo wajibikia Waumini kuyafuata wanapo ingia nyumba za Nabii kwa ajili ya kula na kuwa wakisha wende zao, na juu ya kuwauliza wake zake nyuma ya pazia. Na Sura ikawataka Mamama wa Waumini (wake za Mtume s.a.w.) wateremshe mitandio yao juu ya vifua yao. Na Sura ikazungumza juu ya Saa na vitisho vya Kiyama, na ikatoa nasaha ya kumcha Mwenyez Mungu, na kusema maneno yaliyo sawa, na ikakhítimishia kwa kutaja jukumu la Mwenyezi Mungu alilo libeba mwanaadamu, hali mbingu na ardhi na milima ilishindwa kulibeba.

Kutokana na hayo inaonekana kuwa makusudio muhimu kabisa ya Sura hii ni Maneno Juu ya watoto wa kupanga, na kuivunja ada iliyo kuwa imeenea wakati ule kuharimisha kuwaoa wana wa kupanga ambao ni halali kwao; na ihsani ya Mwenyezi  Mungu kuwafanyia Waumini kwa ushindi kuwashinda washirikina kama alivyo waahidi; na kufafanua sharia aliyo wawekea Mwenyezi Mungu Waumini wanapo ingia nyumba za Nabi s.a.w. ma kuwaharimishia kuwaoa wake zake baada yake, na kuzipanga adabu makhsusi zilizo wakhusu Mamama  wa Waumini, yaani wake za Mtume s.a.w.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa