Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
038

Sura Sad

Aya:

88

Mahali iliteremshwa:

Makka

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT S'AAD 

(Imeteremka Makka) 

Sura hii ni ya thalathini na nane katika sura za Qur'ani Tukufu. Nayo ni Sura ya Makka, na Aya zake ni 88. 

Sura hii inatueleza namna ya inda ya washirikina waliyo kuwa wakiufanyia Wito wa Nabi Muhammad sa.w. na uhasidi wao kwa vile Mwenyezi Mungu alivyo mkirimu kwa kumpa utukufu wa Utume, na kumteremshia Qur'ani. Basi inawajibu kwa yale mawazo ya uwongo walio mnasibishia nayo. Na mebainisha kwamba yaliyo wapelekea kuupiga vita Wito wake kama wafanyavyo Si lolote ila ni dharau ya uwongo, na kupenda kuleta khitilafu na mgawanyo. Na lau kuwa adhabu ya Mwenyezi Mungu inge wateremkia, msimamo wao kwa Mtume s.a.w. usingeli kuwa hivyo ulivyo. Kisha Mwenyezi Mungu amewapigia mifano ya kaumu zilizo kwisha tangulia, ili wapate kuacha inadi na kuleta dhiki, na ili kumpa moyo Mtume wake s.a.w. kufikisha Wito, na hata ange pata taabu zozote na vitimbi vyovyote vya washirikina kwa ajili yake. Na apate kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema alizo mpa, kama walivyo fanya ndugu zake Manabii na Mitume wengine. Na kutokea na haya, anataja marejeo mema aliyo waandalia Mwenyezi Mungu wachamngu, na maangukio maovu aliyo waandalia wenye kuasi. 

Kisha akawakumbusha yaliyo kuwa baina ya baba yao Adam (AS) na adui yake Iblisi, ili wajue kuwa anayo waitia Iblisi kufanya kiburi kwa kupinga kufwata haki ni tabia katika tabia zake Iblisi. Na kupanda kiburi huku ndiko kulikuwa sababu ya kufukuzwa kwake kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu.

Sura imekhitimisha kwa kueleza vilivyo kazi muhimu ya Mtume s.a.w., nayo ni kufkisha Wito, na kwamba yeye hawataki ujira kwa hayo, na yeye hakujileta nafsi yake. Na Qur'ani si chochote ila ni Ukumbusho kwa walimwengu wote. Na bila ya shaka watakuja jua ukweli wa khabari zake baadae.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa