Makka
Sura Al-Mutaffifyn

Aya

36

Mahali iliteremshwa

Makka

SURAT AL-MUT'AFFIFIIN 

(Imeteremka Makka)

Imeanzia Sura hii kwa onyo kali kwa huyo anaye jipimia mwenyewe sawa na akampimia mtu mwingine kwa upungufu; na ikaeleza hayo kwa wayatendayo watu katika kutaka watimiziwe haki zao katika vipimo na mizani, na ikaonya mtindo kama huo kwa kuwa ipo Siku ya Hisabu, na ikathibitisha kuwa vitendo vyao vimedhibitiwa katika daftari la hisabu, ambalo halimkadhibishi ila mwenye kupindukia mipaka, mwenye dhambi aliye zuiliwa na rehema za Mola wake Mlezi, na mwisho wake ni Jahannamu. 

Tena Aya zikawageukia watu wema, zikawatuza nyoyo kwa vitendo vyao, na zikataja neema zao na alama zao, zikiashiria namna moja wapo katika neema hizo, na kwa ajili ya hizo washindanie wanao shindana. Na Aya zikaeleza walio kuwa wakiyafanya makafiri wakosefu kuwafanyia Waumini wanapo waona, au wanapo kuwa Waumini wanapita mbele yao. Na Sura ikakhitimisha kwa kuwatuliza Waumini kwamba Siku ya Kiyama itawafanyia insafu, wao watakuwa katika neema wakiwacheka makafiri, nao wamekaa juu ya makochi wakiwaangalia, na makafiri watalipwa kwa waliyo kuwa wakiyatenda.