Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Chagua Lugha
Taarifa ya Sura
060

Sura Al-Mumtahinah

Aya:

13

Mahali iliteremshwa:

Madina

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT AL-MUMTAH'INAH 

(Imeteremka Madina)

Sura hii imeanza kwa kuwakataza Waumini wasiwafanye urafiki washirikina, ambao ni maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zao wao, kwa kushikilia kwao ukafiri, na kumtoa Mtume wa Mwenyezi Mungu na Waumini kwenye nyumba zao Makka. Na ikaashiria kwamba uadui wa watu hawa kwa Waumini, ulio fichikana, hauwachi kudhihiri pale wanapo wakuta na wakapata nguvu juu yao. 

Kisha Sura ikaingia kubainisha ruwaza njema ya Ibrahim na walio kuwa pamoja naye katika kujitenga na washirikina, na hayo waliyo kuwa wakiyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu, wakitangaza uadui wao kwao mpaka wamuamini Mwenyezi Mungu peke yake. Hayo yanaonyesha kuwa huo ndio mwendo wa wanao taraji kukutana na Mwenyezi Mungu, na wanaogopa adhabu yake. 

Kisha ikabainisha makhusiano yepi yanafaa kuwa nayo na wasio kuwa Waislamu, na yepi hayafai. Ama wale ambao hawatupigi vita katika Dini wala hawasaidii dhidi yetu, basi ni waajibu wetu kuwafanyia wema, na kuwafanyia haki. Ama hao wanao tupiga vita katika Dini, na wakasaidia katika kututoa kwenye nyumba zetu na miji yetu, hao, basi, ndio Mwenyezi Mungu anatukataza kuwafanyia hisani na kukhusiana nao.

Kisha Sura ikabainisha hukumu ya Waumini wanawake walio hamia kwenye mji wa Kiislamu, na wakawaacha waume zao wa kishirikina; na hukumu ya wanawake wa kishirikina ambao waume zao Waislamu wamehama, na hao wanawake wakaachwa katika mji wa shirki. 

Na ikafuatiliza kueleza kutoa utiifu wanawake, kwa walivyo mtolea Mtume s.a.w Kisha Sura ikakhitimisha, kama ilivyo anza, kwa kukataza kuwafanya urafiki maadu walio kasirikiwa na Mwenyezi Mungu, ili kuthibitisha hukumu iliyo kwisha tolewa mwanzo wake, na ikaitilia nguvu katika kuthibitisha kwake.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa