🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
045

Sura Al-Jathiyah

Aya:

37

Mahali iliteremshwa:

Makka

SURAT AL-JAATHIYA 

(Imeteremka Makka)

Imeanzia Sura hii kwa harufi mbili katika harufi za Alifbete, na kubainisha kuwa kuteremshwa Qur'ani kumetokana na Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu Mwenye hikima. Kisha ikazitaja dalili za uumbaji na za kiakili kuthibitisha itikadi ya Imani na kuitia watu waifuate. Hali kadhaalika imekusanya wito kwa wenye kukadhibisha Ishara. Kisha ikaingia kuzihisabu neema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake kwa waja wake; na ikawataka Waumini wawasamehe makafiri wanao kanya Kwani Mwenyezi Mungu peke yake ndiye wa kumlipa kila mtu kwa alilo litenda.

Kisha Sura baada ya hayo ikazungumzia vipi Mwenyezi Mungu alivyo wafadhili Wana Israili kwa kuwapa neema nyingi, na khitilafu zilizo zuka baina yao ambazo Mwenyezi Mungu atazitolea hukumu Siku ya Kiyama. Kisha ikaingia kufarikisha baina ya walio fuata Haki na walio fuata matamanio, wakakanya kufufuliwa, na wakapinga Ishara za uweza kwa kutaka wafufuliwe baba zao! Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuhuisha, na ndiye Mwenye kufisha. Yeye ana ufalme wa kila kitu. Na siku watakapo kusanywa wapotovu kila nafsi itaitwa ikapokee kitabu chake. Hapo watafuzu Waumini na watakemewa walio takabari. 

Sura tena inarejea hadithi ya kule kuikataa kwao Saa ya Kiyama, na kuzikadhibisha Ishara zinazo ionyesha; na vile Mwenyezi Mungu atavyo wasahau wao kama wao walivyo isahau hii Siku. Na ikabainisha kuwa makaazi yao ni Motoni kwa kule kuzikejeli kwao Ishara za Mwenyezi Mungu na kudanganyika kwao na dunia. Na Sura imekhitimisha kwa kumsifu Muumba mbingu na ardhi, Mwenye utukufu kote humo, Mwenye nguvu. Mwenye hikima.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa