Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Chagua Lugha
Taarifa ya Sura
007

Sura Al-Aaraf

Aya:

206

Mahali iliteremshwa:

Makka

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT AL- A'RAAF 

(Imeteremka Makka)

Sura hii imeteremka Makka isipo kuwa Aya nane, nazo ni 163 mpaka 170. Na idadi za Aya zake ni 206.

Mwanzo wa Sura hii ni kuendeleza yaliyo kuja mwisho wa Sura ya Al-Ana'm, na baada ya hayo imeingia kueleza khulka ya kibinaadamu. Ikataja kisa cha Adam na Hawa. na walivyo toka kwenye Bustani kwa kutiwa wasiwasi na Shetani, na ikaeleza huo wasiwasi unaoendelea kwa watu katika mAyazi na chakula. Kisha Aya za Sura hi tukufu, kama sura nyengine za Qur'ani zikaingia kutupia jicho kwenye mbingu na ardhi na viliomo ndani yao, na kuzingatia uumbaji wake wa ajabu.

Kadhaalika Sura hii imeeleza hadithi za Manabii kama Nuhu na Hud na kaumu yake kina A'ad Kisha hadithi ya Saleh na kaumu yake, Thamud, walio sifika kwa nguvu zao na wakapewa utajiri; na hadithi ya Lut na kaumu yake, na ikataja maovu waliyo kuwa wakiyafanya; na hadithi ya Shua'ib na watu wa Madyana. Na baada ya hadithi hizo za kweli Sura imeeleza mafunzo na mazingatio yaliyomo: Naye Subhanahu wa Ta'ala amefuatilizia hayo kwa kisa cha Musa na yaliyo tokea katika mambo ya Firauni.

Na Sura ikakhitimishia kwa kumathilisha nini hali ya mwenye kupewa hidaya khalafu akabanduka kwenye uwongofu akaingia kwenye upotovu kwa kumfwata Shetani, na Sura pia ikamalizia kueleza Wito wa kuendea Haki alio kuja nao Muhammad, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa