Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
020

Sura Ta Ha

Aya:

135

Mahali iliteremshwa:

Makka

SURAT T'AHA 

(Imeterenka Makka)

SURA hii ni ya Makka, isipo kuwa Aya mbili, nazo ni Aya 130 na 131, Hisabu ya Aya zake ni 135. Sura hii imeanza kwa harufi mbili za kuzindua juu ya muujiza wa Qur'ani na kuwazindua wasikilizaji waisikilize. Baada ya harufi hizo mbili cheo cha Qur'ani kimetaijwa, na utukufu wa hii Qur'ani ni utukufu wa Mwenye kuileta, naye ni Mwenyez Mungu, Subhanahu wa Taa'la, Mmiliki mbingu na ardhi, Mwenye kujua siri, na kilicho fichikana kuliko siri. Kisha kimesimuliwa kisa cha Musa (AS) pamoja na Firauni, na vip alipo anza kupewa utume Nabii Musa (AS) Na yametajwa maombi yake kutaka nduguye Harun (AS) awe msaidizi wake wa kumpa nguvu, tena vipi walivyo kutana na Firauni baada ya kitisho cha mkutano wake kwa ajili ya ujeuri wake. Na katika mintarafu ya haya Mwenyezi Mungu Mtukufu amebainisha kuzuka kwa Musa (AS).

Katika Sura hii pana majibizano baina ya Musa na Firauni, tena baina ya Musa (AS) na wachawi. na hali ya Musa ya kuogopa kushindwa mbele ya wachawi, na fimbo yake ilipo zimeza kamba zao, na tena mwisho vipi yalivyo ishia mambo ya wachawi na kuamini kwao, na Firauni kuwaadhibu. Kisha ikatajwa vipi Musa alivyo toka yeye na Wana wa Israili kutokana na Firauni, na vipi alivyo zama Firauni, naye alikuwa kawafuatia baada ya kupasuka bahari: na vipi Musa aliokoka akafika Jabal Tur akawaacha watu wake ili ende kwenye mlima kuzungumza na Mola wake Mlezi. Na Msamaria akawafitini kwa kuwachochea waliabudu sanamu la ndama lililo undwa kwa dhahabu. Na ilikuwa ukipita upepo ndani yake hutoa sauti. Musa alikasirika kwa yaliyo tokea, akamkamata kichwa nduguye akimvutia kwake.

Kisha katika Sura hii tukufu akatokea yaliyo msibu Msamaria. Mwenyezi Mungu Subhanahu amesimulia hadithi ya kuvuka katika hadithi za Musa na nyenginezo. Na mwisho wa Sura pana mausio mema juu ya Subira, na Usamehevu, na Sala. Kisha ikabainishwa kubwatika washirikina katika matakwa yao ya muujiza mwengine usio huu wa Qur'ani; na Subhanahu ameashiria hikima ya kuwatuma Mitume. Tena Sura hii tukufu imekhitimisha kwa kuashiria adhabu watakayo pata makafiri, na malipo mema watakayo pata Waumini.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa