Aya
4
Mahali iliteremshwa
Makka
SURAT QURAISH
(Imeteremka Makka)
Mwenyezi Mungu katika Sura hii anataja neema alizo wafanyia Maqureshi kwa Nyumba yake takatifu ambayo ameilinda na maadui wake, naye akawapa maskani karibu yake wakapata utukufu na amani, na wakawa wanasafiri siku za baridi kwenda Yaman, na siku za joto wakenda Shamu, kwa ajili ya biashara bila ya mtu yeyote kuwaletea maovu, na hali watu jirani zao siku zote wakinyakuliwa. Na neema hizo zinawajibikia kumuabudu huyo aliye kuwa anawalisha wasipate njaa, na akawalinda na khofu.