Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
047

Sura Muhammad

Aya:

38

Mahali iliteremshwa:

Madina

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT MUH'AMMAD 

(Imeteremka Madina) 

Sura hii imeanza mwanzo wake kubainisha kwamba Mwenyezi Mungu amezibatilisha amali za makafiri kwa kuwa wamefuata upotovu, na amewafutia Waumini maovu yao kwa kufuata kwao Haki. Kama ilivyo eleza kwa urefu waajibu wa kuitetea Haki. Na malipo hayo kwa Akhera ni kuingia Peponi Na ikawahimiza Waumini wainusuru Dini ya Mwenyezi Mungu na wapigane kwa ajili yake. 

Na imeweka wazi kwamba wapotovu wakiacha Imani hufanya fisadi katika nchi na wakawatupa jamaa zao. Na inahadharisha juu ya wanaafiki kuwa pamoja na Waumini wakapeleleza siri zao wapate kuwavunja moyo. Na inawatishia wanaafiki kuwa yatachanwa mapazia yao wanayo jifichia, na Mtume wa Mwenyezi Mungu adhihirishe chuki zao. Na inawakataza Waumini wasiwe wanyonge katika kupambana na makafiri, na hali wao ndio watakao shinda, na Mwenyezi Mungu yu pamoja nao, na wala hatawanyima malipo ya kazi yao. 

Kisha Sura imekhitimisha kutaka watu watoe kwa sababu ya Sabili Llah, Njia ya Mwenyezi Mungu, na ikabainisha kwamba mwenye kufanya ubakhili katika hayo basi anajidhuru mwenyewe, na kwamba kuacha kufuata Haki inakuwa ndiyo sababu ya kuhiliki hao wenye kuacha na kuletwa kaumu nyengine zenye kuleta kheri.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa