Aya:
15
Mahali iliteremshwa:
Makka
Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab
SURAT ASH-SHAMS
(Imeteremka Makka)
Mwenyezi Mungu Mtukufu ameapa kuanzia Sura hii kwa vitu kadhaa wa kadhaa miongoni mwa viumbe vyake vitukufu, vyenye kueleza utimilivu wa uweza wake Mwenyezi Mungu Mtukufu na Upweke wake, juu ya kufuzu kwa mwenye kuisafisha nafsi yake kwa Imani na utiifu, na kukhasiri kwa kupinga mwenye kuidhoofisha kwa ukafiri na maasi. Kisha ikaingilia mfano wa Thamudi, kaumu ya Saleh, na yaliyo wafika hao, ili apate kuzingatia kila mwenye inda mwenye kukadhibisha. Kwani hakika wao walipo mkadhibisha Mtume wao, na wakamuuwa yule ngamia, Mwenyezi Mungu aliwaangamiza wote, na Yeye hakhofu matokeo ya kuwaangamiza hao, na aliyo wateremshia, kwani Yeye hasailiwi kwa anayo yatenda, na hakika amewateremshia wanayo stahiki.