🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
023

Sura Al-Muuminun

Aya:

118

Mahali iliteremshwa:

Makka

SURATUL MUUMINUN 

(Imeteremka Makka)

HII NI SURA iliyo teremka Makka. Aya zake ni mia na kumi na nane. Imeanza kwa kuthibitisha mafanikio ya Waumini, na ikafuatia kueleza sifa zao. Kisha ikataja asli ya kuumbwa mwanaadamu, na kubadilika kwake kwa kukua, na kuzalikana vizazi vyake, na baadhi ya mambo yanayo dhihirisha uwezo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. 

Tena zikafuatia hadithi za Manabii zinazo fanana kwa umoja Wa ujumbe na umoja Wa binaadamu, ijapo kuwa watu wange khitalifiana baina ya wanao kubali na wanao kengeuka. Na sura hii imeeleza khabari za mwenye kutaka uwongofu, na mwenye kupotoka, na msimamo wa washirikina mbele ya Nabii s.a.w. Tena ikaingia kueleza yanayo onekana ya uwezo wa Mwenyezi Mungu katika hukumu za kumuumba mwanaadamu. 

Na Mwenyezi Mungu Subhanahu kaingia kuwauliza watu wamjibu kwa kutumia akili zao za maumbile kwa yanayo thibitisha kuwepo kwake, na kuthibitisha Ungu wake. Kisha Sura hii ikaeleza hali za watu itakavyo kuwa Siku ya Kiyama, na kwamba wao watahisabiwa, na watafanyiwa uadilifu. Tena Sura inakhitimisha kubainisha Utukufu wake Subhanahu wa Taa'la, na kumnabihisha Nabii wake aombe maghfira na rehema kutokana na Mbora wa wenye kurehemu.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa