Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
048

Sura Al-Fat-H

Aya:

29

Mahali iliteremshwa:

Madina

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT AL FAT-H' 

(Imeteremka Madina)

Imeanzia mwanzo wake Sura hi kwa kutaja Ushindi ulio wazi, alio msahilishia Mwenyezi Mungu Mtume wake, na imeelezea athari zake kubwa katika kueneza Uislamu na kuwatukuza Waislamu, na kuziimarisha nyoyo za Waumini iliwazidi Imani, na kuadhibiwa kwa wanaafiki na washirikina, kwa shaka shaka zao juu ya nusura ya Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake. Na imetaja kuwa Mtume Muhammad s.a.w. ametumwa kuwa ni mwenye kushuhudia, na mwenye kubashiria, ili ithibiti Imani ya Mwenyezi Mungu. 

Tena Sura ikaingia kueleza kusimulia kuungwa mkono Mtume na watu wa kweli wa kutimiza ahadi, na ikabainisha uwongo wa udhuru walio toa walio kwenda kinyume na Mtume wasitoke naye kwenda pambana na maadui, na ambao walibaki nyuma kwa kudhania kwao kuwa Mwenyezi Mungu hatampa nusura Mtume, na ikaeleza kuwa kutaka kwao kutoka naye ni kwa sababu ya kupata ngawira.

Tena Sura imebainisha kuwa watakuja takiwa kupigana na kaumu wakali na wenye nguvu, na kwamba hapana makosa kuacha kwenda vitani kwa udhuru wa kweli. Kama ilivyo weka wazi ukubwa wa kheri alizo waahidi Mwenyezi Mungu wale alio furahi nao katika kumuunga mkono Mtume s.a.w. kwa Ridhwani. Imezungumzia juu ya kukimbia kwao makafiri na kushindwa kwao walipo pigana na Waumini, ikaeleze hikima ya Mwenyezi Mungu kuwazuia makafiri wasiwapige Waumini, na kuwazuia Waumini wasiwapige makafiri wakati wa kutekwa Makka. 

Na mazungumzo yakamalizikia kwa kubainisha kwamba Mwenyezi Mungu ameitimiza ndoto aliyo iota Mtume wake ya kuingia katika Msikiti Mtakatifu,nakwamba Muhammad na walio amini pamoja naye ni wakali kwa makafiri lakini ni wapole, wanaoneana huruma Wao Kwa wao. Na ikabainisha alama za kuwajuulisha Waumini, na sifa zao katika Taurati na sifa zao katika Injili, na Mwenyezi Mungu kawaahidi walio amini na wakatenda mema msamaha mkunjufu, na ujira mkubwa.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa