Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
050

Sura Qaf

Aya:

45

Mahali iliteremshwa:

Makka

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT QAAF 

(Imeteremka Makka)

Mwanzo wake Sura hii inasimulia kuthibiti Utume wa Muhammad s.a.w. na wanavyo kanya makafiri kuja Mtume kati yao, na kuona muhali kufufuliwa baada ya kwisha geuka dongo. Na ikaeleza Ishara za uumbaii zinazo onyesha dalili ya kwamba Mwenyezi Mungu hashindwi kuwafufua watu baada ya kufa kwao, na hali Yeye ndiye aliye waumba hapo kwanza, na anajua yanayo wapitikia katika nafsi zao. 

Na Yeye anavisajili vitendo vyao na maneno yao katika Daftari lenye kuhifadhi hata dogo. Na Sura imebainisha kwamba majaribio ya makafiri Siku ya Kiyama kutaka kuukataa ukafiri walio kuwa nao duniani, ati kwa kusingizia walikuwa ni wafwasi tu wa Mashetani hayatawaletea nafuu yoyote. Kwani mwisho wa mjadala wao ni kutumbukizwa wote katika Moto, na huku Mwenyezi Mungu anawafadhili Waumini kwa kuwapa neema za milele katika Pepo. Kisha Sura inamalizikia masimulizi yake kwa kumuamrisha Mtume s.a.w. avumilie maudhi ya makafiri ambao hawakuzingatia yaliyo wapata walio kadhibisha katika kaumu zilizo kuwa kabla yao, na kumwelekeza Mtume s.a.w. athibiti juu ya ibada ya Mwenyezi Mungu, na kutilia mkazo hili jambo la kufufuliwa, na kumliwaza Mtume s.a.w. kwa kuwa yeye ni mwenye kuwakumbusha Waumini, wala si mtawala wa makafiri.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa