Ingia
🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
013

Sura Ar-Raad

Aya:

43

Mahali iliteremshwa:

Madina

SURAT AR-RAA'D 

(Imeteremka Madina)

"Surat Ar Raa'd" ni Sura ya Madina, na imeitwa "Raa'd" kwa kusimuliwa kwamba Radi (inamsabihi) inamtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na hisabu za Aya zake ni arubaini na tatu. Imeanza Sura hii kwa kubainisha cheo cha Qur'ani Tukufu, na kwamba imeteremshwa kwa Wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. 

Kisha ikabainisha uwezo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika ulimwengu wote, na ikazindua kueleza mambo yaliyo umbwa na yenye manufaa Kisha ikatoka kubainisha uwezo wake Mwenyezi Mungu wa kuumba, ikaingia kubainisha uwezo wake kurejesha tena na kufufua, na ujuzi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu wa kila kitu, na kubainisha kudra yake ya kuadhibu duniani, na kwa hivyo yaweza kukisiwa adhabu ya Akhera. Kisha Sura hii ikaelekeza nadhari zizingatie maajabu ya ulimwengu yaliyo zagaa. Baada ya hayo Mwenyezi Mungu Mtukufi amezieleza hali za watu katika kupokea kwao uwongofu wa Qur'ani. 

Kisha akataja sifa za Waumini katika makhusiano yao ya kibinaadamu, na tabia za makafiri na karaha yao kushikilia kutaka miujiza isiyo kuwa hii Qur'ani juu ya ubora wake wa cheo, na ikataja kejeli zao kwa Mtume wao. Na ikamueleza Mtume kuwa Mitume wa kabla yake pia walifanyiwa kejeli! Na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mwenye kusimamia vitu vyote na nafsi zote, na kwamba Yeye ni Mwenye kumlipa kila mtu kwa anavyo stahiki, na kwamba Qur'ani ndio muujiza mkubwa kabisa utakao baki mpaka Siku ya Kiyama, na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye anaye wapa nguvu Mitume wake kwa miujiza aitakayo. Na ikiwa hao washirikina wanakanya Utume wa Nabii huyu, basi Mwenyezi Munge Mwenyewe anashuhudia ukweli wake, na Yeye ni Mwenye kutosheleza kwa hayo.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa