Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
057

Sura Al-Hadyd

Aya:

29

Mahali iliteremshwa:

Madina

SURAT AL-H'ADIID 

(Imeteremka Madina) 

 Sura hii imeanzia kwa kueleza kwamba wote walioko mbinguni na katika ardhi wamemsabihi na kumtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu na kika kisicho kuwa laiki naye. Kisha ikafuatiliza hayo kwa kuelekeana na kusabihi huko ufalme wa mbingu na ardhi, na kuvizunguka vyote hivyo na kuviendesha. Kisha Sura ikaamrisha Imani ya Mwenyezi Mungu, na kutoa katika njia yake, na ikabainisha khitilafu za daraja za kutoa kwa mujibu wa kukhtalifiana haja ziliopo na dharura zake. Kisha ikaeleza sura ya Waumini Siku ya Kiyama, inavyo tangulia nuru yao mbele yao na pembezoni mwao: na sura ya wanafiki wanavyo waomba Waumini wawangojee ili nao wapate mwangaza kutokana na nuru yao. Na baina yao umesimamishwa ukuta wenye mlango. Ndani yake ipo rehema, na nje yake upande wa mbele yake ni adhabu.

Na Sura ikaingia baada ya hayo kuwahimiza Waumini wanyenyekee kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu, na Haki aliyo iteremsha. Na inawaonyesha vyeo vya wanao sadiki wanaume na wanawake mbele ya Mola wao Mlezi; na mwisho wa Makafiri wanao kadhibisha ni katika Jahannamu. Na inapiga mifano ya udhalili wa dunia na hizo starehe zake, na ukubwa wa Akhera na neema na adhabu zilioko huko. 

Na Sura inataka watu wawanie kushindania maghfira kwa Mwenyezi Mungu, na inazituza nafsi kwamba kila kinacho msibu mtu ikiwa kheri au shari kimeandikwa katika Kitabu kilichoko kwa Mwenyezi Mungu, ili nyoyo zinyenyekee kwa hukumu ya Mwenyezi Mungu. Kisha ikasimulia khabari za kuwatuma Mitume na kuwafuatiliza mmoja baada ya mmoja wakipewa nguvu kwa hoja na Vitabu, na njia za nguvu na vitendo, ili watu wasimamishe uadilifu. 

Kisha Aya ikakhitimisha kwa kuwaita Waumini wamche Mungu, na ikawaahidi kuwa watapewa rehema maradufu na watafanyiwa hisani ya kufadhiliwa, ambayo hapana mwenye kuiweza hata kidogo ila Mwenyezi Mungu. Kwani hakika fadhila zote zimo katika mkono wa Mwenyezi Mungu,  humpa amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye fadhila kuu.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa