Aya:
4
Mahali iliteremshwa:
Makka
Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab
SURAT AL-IKHLAS'
(Imeteremka Makka)
Nabii s.a.w. aliulizwa khabari za Mola wake Mlezi, akaamrishwa katika Sura hii ajibu kwamba Yeye ni Mwenye kukusanya sifa zote za ukamilifu, ni Mmoja, wa Pekee Mwenye kukusudiwa daima katika haja, Mwenye kujitosha hamhitajii yeyote nwenginewe, ametakasika na kuwa na mfano, hakuzaa wala hakuzaliwa, wala hana mwenzie katika viumbe vyake.
Michango ya kila mwezi hutusaidia kuboresha Quran.com na kuendeleza shughuli zetu, ili tuweke mkazo mdogo kwenye ukusanyaji wa fedha na zaidi kwenye kuleta athari chanya Jifunze zaidi