Ingia
Ingia
Ingia
Chagua Lugha
Taarifa ya Sura
043

Sura Az-Zukhruf

Aya:

89

Mahali iliteremshwa:

Makka

Ali Muhsin Al-Barwani - Tarjuma ya Kiswahili ya Al-Muntakhab

SURAT AZZUKHRUF 

(Imeteremka Makka)

Imeanzia Sura hii kwa harufi mbili za alifbete, na ikafuatia kwa kuitaja Qur'ani na kueleza cheo chake kwa Mwenyezi Mungu. Kisha Sura ikaingia kubainisha msimamo wa wale wanao zifanyia maskhara Risala za Mitume wao, na ikazileta dalili nyingi za kuthibitisha Imani ya Mwenyezi Mungu pekee. Na juu ya hoja hizo wao wakamzulia Mwenyezi Mungu kuwa ana washirika, na wakamfanya kuwa ana watoto wa kike, na wao wanao wa kiume. Na walipo ishiwa na hoja wakashikilia mila za baba zao.

Kisha Sura ikasimulia kisa cha Ibrahim, na ika fuatiliza kule kuyaona makuu makafiri wa Makka ya kwamba Qur'ani iliteremka juu ya Muhammad, wala isiteremke juu ya mmoja katika wakuu wa miji yao miwili. Hayo ni kama kwamba wao ndio wanao zigawanya fadhila za Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu alikwisha wagawia maisha yao ya duniani, kwa kuwa wao wenyewe wameshindwa hayo. 

Kisha Sura ikathibitisha kwamba lau kuwa si kuchukia wasije watu wote wakakufuru basi bila ya shaka angeli mpa kafiri starehe na mapambo na uzuri wote wa duniani. Kadhaalika Sura imebainisha kwamba mwenye kupuuza Haki Mwenyezi Mungu humsalitisha na Shetani amwongoze kwenye maangamio. Kisha Sura inasimulia kisa cha Musa na Firauni, na alivyo ghurika Firauni na ufalme wake, na yaliyo mteremkia Firauni na kaumu yake ya mateso ya Mwenyezi Mungu. Na hayo akafuatiwa kutajwa Bi Maryamu, na kwamba yeye ni mja aliye neemeshwa na Mwenyezi Mungu, na akawaita watu wende kwenye Njia iliyo Nyooka. 

Na baada ya kuonya kwa adhabu ya Siku ya Kiyama itayo wapata walio dhulumu, na kubashiriwa Waumini kuwa watapata Pepo ambayo ndani yake macho yao yatatua, Sura inakhitimisha kueleze kuwa Ufalme wa Mwenyezi Mungu umeenea kote, na hao walio washirikisha naye hawanalo wawezalo. Basi, ewe Muhammad! Wapuuzilie mbali, na useme: Salamu! Watakuja jua!

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Changia
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Quran.AI
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa