Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
053

Sura An-Najm

Aya:

62

Mahali iliteremshwa:

Makka

Ali Muhsin Al-Barwani - Swahili Translation of Al-Muntakhab

SURAT ANNAJM 

(Imeteremka Makka)

Kiapo mwanzo wa Sura hii kinadhihirisha ukweli wa Mtume s.a.w. katika anayo yasimulia ya khabari za Wahyi (Ufunuo) na anayo yafikisha kutokana na huo ufunuo. Hakupoteza kitu katika hayo wala hakukosea. Na Mtume s.a.w. amesema kweli katika aliyo yazungumzia juu ya safari yake ya kwenda mbinguni, katika hayo yaliyo tokea ya Miraji, jicho lake halikuhangaika wala halikuruka mpaka.

Kisha Sura inaingia kueleza uchache wa akili za makafiri kwenda kuabudu masanamu waliyo yaunda wenyewe kwa mikono yao, wakayaita majina yao wenyewe, kama walivyo waita Malaika kuwa ati ni wanawake, baada ya kumfanya Mwenyezi Mungu ana mabinti, na wao wenyewe wawe na watoto Wa kiume.

Kisha Sura inamtaka Mtume s.a.w. awapuuze, na amwachilie mambo yao Mwenyezi Mungu Mwenye kumiliki na kuumba vyote viliomo mbinguni na kwenye ardhi. Na Yeye ndiye atakaye mlipa muovu kwa uovu wake, na mwema kwa wema wake. Naye ndiye Mjuzi kabisa wa yote yanayo pita kwa viumbe vyake na hali zao. Yakafwatia nayo kulaumiwa anaye kanya kuhisabiwa kila mtu kwa vitendo vyake, kama yalivyo kwisha pita kwa sharia zilio tangulia, na ikasimuliwa na Vitabu vya Musa na Ibrahim. Na Aya hizi zimethibitisha maana haya yaliyo elezwa katika uwezo na Ishara za Mwenyezi Mungu katika mataifa yaliyo kwisha tangulia.

Kisha Sura inakhitimisha kwa kuweka wazi kwamba Qur'ani ni onyo miongoni mwa maonyo walio onywa kwayo kaumu zilizo kwisha tangulia, ili wapate kutahadhari na Siku ya Kiyama ambayo imekaribia wakati wake. Na Sura inawalaumu makafiri wanao ikataa Qur'ani kwa kughafilika kwao huko, na wakawa wanacheka badala ya kulia na kuwaidhika kwa Qur'ani. Na ikawataka Waumini wamsujudie Mwenyezi Mungu aliye iteremsha na wamuabudu Yeye tu.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa