🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
🎯 Endelea kufuatilia!
Unda Lengo Langu
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
030

Sura Ar-Rum

Aya:

60

Mahali iliteremshwa:

Makka

SURAT AR-RUM 

(Imeteremka Makka)

SURA hii imeanza kutaja kushindwa kwa dola ya Rumi, na ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa Waumini kwamba atawapa ushindi kuwashinda Waajemi, na ikawataka watu wafikiri juu ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu, na watembee katika ardhi wapate kuujua mwisho wa makafiri walio iamirisha ardhi zaidi kuliko walivyo iamirisha wao Makureshi. 

Na Sura hii imeeleza hali ya watu Siku ya Kiyama, na ikasifu kutakasa kwa Waumini kumtakasa Mwenyezi Mungu, na wanavyo muabudu Yeye asubuhi mapema na jioni, na adhuhuri na alasiri. Na ikanabihisha dalili za Upweke wake Mwenyezi Mungu kwa kupishana zamu usiku na mchana, na kukhitalifiana lugha, na mambo yanayo onekana ya ulimwengu katika mbingu na ardhi. Na ikapiga mifano ambayo inayo onyesha upotovu wa shirki, na ikawakumbusha watu vipi Mwenyezi Mungu alivyo waumba wao na akawaneemesha, na kuvitia nguvu viungo vya ukoo, na kushikamana kwa ujamaa, na ikashughulikia mambo ya sharia, ikaharimisha riba, na ikalazimisha Zaka, na ikahimiza kuwafanyia wema jamaa.

Kisha Mwenyezi Mungu Subhanahu akawaneemesha waja wake na akawataka washike Dini na utiifu, na akawataka waangalie katika ulimwengu yale maajabu yake yanayo onyesha ukomo wa nguvu na uweza wake. Na akabainisha mabadiliko ya binaadamu anavyo geuka mpaka akafikia umri wa ukongwe kabisa. 

Na Aya za mwisho zimegusia Siku ya Kiyama na jinsi washirikina wana vyo ikanya Na Sura ikakhitimishia kwa kumnasihi Mtume s.a.w. athibiti juu ya Haki na avumilie kwa yanayo mfika, kwani ahadi ya Mwenyezi Mungu inakuja tu bila ya muhali wowote.

He has revealed to you ˹O Prophet˺ the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa