Makka
Sura Al-Waqiah

Aya

96

Mahali iliteremshwa

Makka

SURAT AL-WAAQIA'H 

(Imeteremka Makka)

Sura hii imeanzia kwa kusimulia Tukio la Kiyama, na matokeo yatayo ambatana na Tukio hilo. Kisha ikasimulia kuwa viumbe Siku hiyo watakuwa namna tatu. Ikafuatia hayo kwa kufafanua kwa kutosha walio andaliwa kila fungu katika hao, ikiwa ni neema zinazo wafikiana na cheo chao, au ni adhabu inayo nasibiana na ukafiri wao na uasi wao.

Kisha Aya zikaweka wazi baada ya hayo yanayo onekana katika neema za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na athari za uweza wake katika viumbe, na makulima, na maji, na moto; na yanayo hitajika kutokana na athari hizi kumsabihi Mwenyezi Mungu Mtukufu na kumtakasa.