Sura Ar-Rahman

Aya

78

Mahali iliteremshwa

Madina

SURAT ARRAH'MAN 

(Imeteremka Madina)

Sura hii imeingia kuzihisabu fadhila na neema za Mwenyezi Mungu, kwa kuanzia baada ya kumtaja Arrah'man, Mwingi wa Rehema, kwa kutaja neema yake tukufu kabisa, nayo ni Kufunza Qur'ani Tukufu. Tena Aya zikaendelea kuzieleza hizo neema kwa namna ya kuweka wazi utukufu wa Mwenye kuziumba, aliye tukuka shani yake; na inadhihirisha uweza wake na ufalme wake juu ya wanaadamu na majini katika mbingu na ardhi. 

Na inaeleza adhabu za wakosefu na wanao kadhibisha katika Jahannamu, na ikafafanua neema za wachamngu Peponi. 

Na Sura ikakhitimisha kwa kumtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kumsifu. 

Na Sura imeikariri Aya isemayo "Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?" mara thalathini na moja, katika mpango wa ki- Qur'ani kukariri kunako pendeza kama inavyo wafikiana na haja. Kila moja katika hizo Aya inawagonga hao wakanushaji kwa kuzikadhibisha kwao neema za Mwenyezi Mungu katika Aya iliyo kabla yake.