Mpaka ilipokuja amri yetu, na tanuri ikafoka maji, tulisema, "Pakia humo katika kila kitu, jozi mbili ya dume na jike, na ahali zako, isipokuwa wale ambao imekwishawapitia hukumu, na watu walioamini." Na hawakuamini pamoja naye isipokuwa wachache tu.