Na walipo toka kupambana na Jaluti na majeshi yake walisema: Mola wetu Mlezi! Tumiminie subira, na isimamishe imara miguu yetu, na utusaidie tuwashinde watu Makafiri--
Nawe hukuudhika nasi ila kwa kuwa tumeziamini Ishara za Mola Mlezi wetu zilipo tujia. Ewe Mola Mlezi wetu! Tumiminie uvumilivu na utufishe hali ni Waislamu.
–Sura Al-A'raf [7:126]
اشرح لي صدري ٢٥ ويسر لي امري ٢٦ واحلل عقدة من لساني ٢٧ يفقهوا قولي ٢٨