٣٣

Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
٣٤
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
٣٥
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
٣٦
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
Notes placeholders