Hakika, wale ambao Malaika wanawafisha hali ya kuwa wamezidhulumu nafsi zao, watawaambia: 'Mlikuwa katika nini?' Watasema: 'Tulikuwa tumefanywa kuwa wanyoge katika ardhi.' Watawaambia: 'Kwani ardhi ya Mwenyezi Mungu haikuwa na wasaa, mkahamie humo?' Basi hao makazi yao ni Jahannam, nayo ni marejeo mabaya kabisa.