Miongoni mwa Mayahudi wamo wanaopotosha maneno kuyatoa pahali pake, na husema: 'Tumesikia na tumeasi, na sikia bila ya kusikizishwa.' Na husema: "Raai'naa", kwa kuzipotoa ndimi zao na kuitukana Dini. Na lau kama wangelisema: "Tumesikia na tumetii, na usikie na "Undhurna (utuangalie)," ingelikuwa heri kwao na ya unyoofu zaidi. Lakini Mwenyezi Mungu aliwalaani kwa kufuru yao; basi hawaamini isipokuwa wachache tu.