Na mkihofia kuwepo mfarakano baina ya wawili hao, basi mtumeni mpatanishi kutoka kwa jamaa za mume, na mpatanishi kutoka kwa jamaa za mke. Ikiwa wanataka kutengeneza mambo, Mwenyezi Mungu ataleta maafikiano kati yao. Hakika, Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye habari zote.