Na kusema kwao: 'Hakika, sisi tulimuua Masihi Isa, mwana wa Maryam, Mtume wa Mwenyezi Mungu.' Nao hawakumuua wala hawakumsulubisha, bali walifananishiwa tu. Na hakika wale waliohitilafiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana elimu yoyote nayo isipokuwa ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuua kwa yakini.