Enyi mlioamini! Muaminini Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Kitabu alichokiteremsha juu ya Mtume wake, na Kitabu alichokiteremsha kabla yake. Na anayemkufuru Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume wake, na Siku ya Akhera, basi hakika amekwishapotea kupotea kwa mbali.