Na ni vya Mwenyezi Mungu tu vyote vilivyo katika mbingu na vilivyo katika ardhi. Na kwa hakika tuliwausia wale waliopewa Kitabu kabla yenu, na nyinyi pia, kwamba mumche Mwenyezi Mungu. Na mkikufuru, basi ni vya Mwenyezi Mungu vilivyo katika mbingu na vilivyo katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosheleza, Msifiwa.