Na hakika nitawapoteza, na nitawatia matamanio, na nitawaamrisha, basi hakika watakata masikio ya wanyama, na nitawaamrisha, basi hakika watabadili aliyoumba Mwenyezi Mungu. Na mwenye kumfanya Shetani kuwa ni rafiki mwandani badala ya Mwenyezi Mungu, basi hakika amehasiri hasara ya dhahiri.