Na Mwenyezi Mungu amewajaalia majumba yenu yawe ni maskani yenu, na amewajaalia kutokana na ngozi za wanyama, nyumba mnazoziona nyepesi wakati wa safari zenu na wakati wa kutua kwenu. Na kutokana na sufu zao, na manyoya yao, na nywele zao, mnafanya vyombo na mapambo ya kutumia kwa muda.