Yeye ndiye Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu isipokuwa Yeye tu. Mfalme, Mtakatifu, Mwenye salama, Mtoaji wa amani, Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo yake, Mwenye nguvu, anayefanya analolitaka, Mkubwa. Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayomshirikisha nayo.