Enyi mlioamini, msiingie katika nyumba za Nabii isipokuwa mpewe ruhusa kwenda kula chakula, siyo kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni, na mkishakula, tawanyikeni, wala msiweke hapo mazungumzo. Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi, lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa jambo la haki. Na mnapowauliza wakeze haja, waulizeni kwa nyuma ya mapazia. Hivyo ndivyo usafi zaidi kwa nyoyo zenu na nyoyo zao. Wala haikufailiini kumuudhi Mtume wa Mwenyezi Mungu, wala kuwaoa wake zake baada yake kabisa. Hakika jambo hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.