Na bila ya shaka tuliwaweka vizuri siyo kama tulivyokuwekeni nyinyi, na tuliwapa uwezo wa kusikia, na kuona na ufahamu wa nyoyo. Na hayakuwafaa uwezo wao wa kusikia, na kuona na ufahamu wa nyoyo kwa lolote. Kwani hao walikuwa wakizikataa Ishara za Mwenyezi Mungu, na yale waliyokuwa wakiyafanyia masihara ndiyo yakawafika.