Au je, wanasema hawa washirikina miongoni mwa watu wa Nūḥ, kwamba Nūḥ, amezua neno hili? Waambie, «Nikiwa nimemzulia urongo Mwenyezi Mungu hilo, basi ni juu yangu mimi, peke yangu, dhambi ya hilo; na nikiwa ni mkweli, basi nyinyi ndio wahalifu wenye dhambi, na mimi niko mbali na ukfiri wenu, ukanushaji wenu uhalifu wenu.