Na tukawafuatishia nyuma yao, Isa mwana wa Maryam akiyasadikisha yale yaliyokuwa kabla yake katika Taurati, na tukampa Injili iliyo na uongofu ndani yake, na ni nuru, na inayosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake katika Taurati, na ni uwongofu na mawaidha kwa wacha Mungu.