Они посчитали, что не будет искушения, и потому стали слепы и глухи. Затем Аллах принял их покаяние, после чего многие из них снова стали слепы и глухи. Аллах видит то, что они совершают.
Тафсиры
Слои
Уроки
Размышления
Ответы
Кираат
Хадис
Na walidhania waasi hawa kwamba Mwenyezi Mungu Hatawatia mkononi kwa kuwaadhibu kwa sababu ya kuasi kwao na kutakabari kwao, ndipo wakaendelea katika matamanio yao na wakawa vipofu wa kutouona uongofu na wakawa viziwi wa kutoisikia na kutonufaika na haki. Hapo Mwenyezi Mungu Aliwateremshia adhabu Yake, wakatubia na Mwenyezi Mungu Akawakubalia toba zao. Kisha wengi wao walikuwa vipofu na viziwi baada ya kubainikiwa na haki. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona matendo yao, mazuri na mabaya, na Atawalipa kwa matendo yao hayo.