Los creyentes [en el Islam], los judíos, los sabeos[1] y los cristianos, quienes crean en Dios [sin asociarle nada] y en el Día del Juicio y obren rectamente, no habrán de sentir temor ni tristeza. 1
Tafsires
Capas
Lecciones
Reflexiones.
Respuestas
Qiraat
Hadith
Hakika wale walioamini (nao ni Waislamu), Mayahudi na al- Ṣābiūn (Masabai, nao ni watu waliosalia kwenye umbile lao na hawana dini fulani waifuatayo), Wanaswara (nao ni wafuasi wa al-Masīḥ), waliomuamini Mwenyezi Mungu miongono mwao Imani kamilifu, nayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu, kumuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na yale aliyokuja nayo, wakaiyamini Siku ya Mwisho na wakatenda matendo mema, basi hao hawatakuwa na hofu yoyote juu ya janga la Siku ya Kiyama wala wao hawatakuwa na huzuni juu ya yale waliyoyaacha nyuma yao duniani.